ads

Breaking News

Mifuko ya plastiki inayoaminika kuwa na mabaki ya viungo na mabaki ya miili ya binadamu Dar es Salaam



viungo3

Mifuko ya plastiki inayoaminika kuwa na mabaki ya viungo na mabaki ya miili ya binadamu ikiwa imetelekezwa kwenye eneo la machimbo Mbweni Mpiji Magohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam janaMifuko ambayo imesheheni mabaki ya kile kilichoelezwa kuwa ni mabaki ya miili ya binadamu ambayo ilitupwa na kugundulika mapema leo kwenye eneo lamachimbo Mbweni Mpiji Magohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam
Kwa mjibu wa Afisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema viungo hivyo vya binadamu vilivyokutwa ni miguu,vidole ambavyo vilikutwa vikiwa vimefungwa ndani ya mifuko.
Hata pamoja na viungo hivyo pia vifaa vya upasuaji vimekutwa zikiwemo glovuzi.
Mtu mmoja anashikiliwa kuhusishwa na tukio hilo ambaye ni dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo lililobeba viungo hivyo vya binadamu.
Haijafahamika mara moja miili hiyo ya binadamu imetolewa wapi na ilipelekwa eneo hilo kwa lengo gani

 

viungo


 SASA Habari zimethibitisha kwamba masalia ya viungo vya binadamu vilivyotupwa maeneo ya Bunju yametoka chuo cha udaktari IMTU kilichopo Mbezi baada ya wanafunzi kumaliza kutumia kwa mazoezi. Viungo hivi vilitupwa baada ya Kukosa pesa za kuteketeza kwenye tanuri maalum.

No comments