ads

Breaking News

Desire Luzinda: Picha ya utupu imenipa umaarufu ambao sikuwahi kuupata kupitia muziki, adai yeye ni tishio kwa Kim kardashian

desire2
Licha ya kuwa tukio la kuvuja kwa picha za utupu limempa picha mbaya kwa jamii muimbaji wa Uganda Desire Luzinda, lakini upande mwingine limemuongezea umaarufu mkubwa kwa muda mfupi ambao hakuwahi kuupata kupitia muziki wake ambao amekuwa akiufanya miaka mingi.
Sasa amefahamika zaidi ndani na nje ya Uganda.Kwa mujibu wa Bigeye ya Uganda, Luzinda amewaambia marafiki zake jinsi alivyokuwa maarufu kupitia picha moja tu ya utupu.
“Nimepoteza muda mwingi kufanya muziki, nimejitahidi sana kutoa hits. Yote hiyo ilikuwa kazi ngumu, lakini picha moja tu ya utupu Uganda nzima inanizungumzia mimi. Nimeweza hata kwenda BBC na Daily Mail. Muziki wangu usingeweza kunifikisha kwenye hizo sehemu lakini mwili wangu umeweza.” Inadaiwa Luzinda aliwaambia marafiki zake.
Aliongeza, “Nafikiria mtu kama Kim Kardashian anaogopa kwasasa. Vinginevyo, kwanini akimbilie kupiga picha za utupu wakati ambao BBC imenihoji mimi. Anahofia. Hataki kukubali ukweli kwamba sisi watu weusi tuna miili mizuri na tunavutia. Kama yeye ame ‘break the Internet, mimi nitaivunja vizuri zaidi.”
desire n Sporah
“Kuna vingi tunavyofanana, lakini lazima niseme, mimi ni mzuri zaidi, Wakati ambapo mkanda wangu wa ngono utakapotoka, mkanda wa ngono wa Kim utapotea kwasababu wangu umejaa mvua za elnino. Lakini ngoja niende taratibu, muda ukifika, sitavunja tu internet, nitaifunga internet na ‘bombastic sextape’ yangu.”
Wakati huo huo Luzinda ameingia studio kurekodi wimbo uitwao ‘Apology’, ukiwa ni maalum kwaajili ya kuwaomba radhi mashabiki wake, marafiki na familia.

No comments