ads

Breaking News

Picha, Lil Wayne Sasa Kwenye Mapenzi Mazito Na Aliyekuwa Mpenzi Wa Msanii The Dream,Angalia Alivyomchana Mpenzi Wake

Kama ulidhani mahusiano ya rapper Lil Wayne na msanii wa Rnb Christina Milian ni ya kibiashara zaidi basi kwa sasa imafahamika kuwa wawili hawa wako kwenye mahusiano ya kimapenzi na tayari wameanza kuonyesha watu baada ya kuonekana kwenye tuzo za ESPYS. Wayne alimshika mkono kwa nguvu Christina Milian wakati wanaingia pamoja kwenye tuzo hizo  na hawakuona aibu kurekodiwa wakiwa wawili na camera za show hio.
Awali Christina Milian alikuwa na msanii The Dream na mahusiano yao yalizaa mtoto moja, hivi karibuni ameachana na mchumba wake Jas Prince. Hivi karibuni Lil Wayne alimdiss mchumba wa Christina ‘Jas Prince’ kwenye wimbo wake kwa kusema  “I’ll take your Tina” (Short for Christina), and “She needs a king, f-ck a prince” (in reference to Jas Prince).
Jas Prince anasema ameumizwa na kitendo cha Lil Wayne kumtukana na kumchukua mpenzi wake kwani walikuwa marafiki na yeye ndiye alimtambulisha Drake kwa Lil Wayne na ndiye alimsaidia Christina kupata record lebel ya Young Money mwaka 2012.
Lil-Wayne-and-Christina-Milian-at-the-ESPYS Lil-Wayne-and-Christina-Milian-ESPY

No comments