ads

Breaking News

Baada ya Ciara na Future kuachana, waanza mapambano

Rapper Future na Ciara ambao wamepata mtoto miezi mitatu tu iliyopita wameshindwa kupika na kula katika chungu kimoja na hatimaye wamepigana chini.
Kwa mujibu wa TMZ, wasanii hao ambao walikuwa wachumba waliovishana pete ya gharama waliachana kufuatia tabia za Future kuendekeza michepuko hali iliyompelekea Ciara kuvua pete hiyo kama mwiba uliokuwa unamchoma kidoleni.
Masaa kadhaa baada ya wawili hao kutangaza kuachana rasmi, imeelezwa kuwa mapambano mengine yameanza kuhusu mtoto na tayari Ciara ameshaanza michakato ya kisheria kumlinda juu ya malezi ya mwanae.
Ciara amepost picha ya mwanae huyo wa kiume akiwa amemuweke mkono wake hali iliyotafsiriwa kama ndicho kitu cha thamani alichobaki nacho katika penzi lao.


Future alikuwa tayari ana wanawake watatu aliozaa nao lakini Ciara aliamini mapenzi hayapimwi kwa kuangalia historia

No comments