ads

Breaking News

Hii ndio Idadi mpya iliyotajwa ya miili iliyopatikana katika ajali ya Ndege ya Malaysia.

malay2
Wafanyakazi wa dharura wa Ukraine wanasema wamekuta miili ya watu 196 katika eneo ilipotokea ajali ya ndege yaMalaysia ya MH17.

Jumla ya watu 298 walikuwemo ndani ya ndege hiyo wakati iliporipotiwa kutunguliwa katika eneo linaloshikiliwa na waasi la ukanda wa Donetsk siku ya Alhamis.
Nchi za Magharibi zimekosoa vikwazo vinavyowekwa katika eneo ilipotokea ajali na kuitaka serikali ya Urusi kuweka shinikizo kwa serikali ya Ukraine kuruhusu kuingia katika eneo hilo.
malay
Waangalizi wa kimataifa wanatarajia kutembelea eneo hilo tena hapo baadae.
Serikali zote Ukraine na Urusi zimetuhumiana kwa kuitungua ndege hiyo iliyokuwa ikiruka kutoka Amsterdam kwenda Kuala Lumpur.

No comments