ads

Breaking News

jana ilikuwa ni siku ya wanaotumia mkono wa kushoto duniani, fahamu maajabu ya watu hao kama Obama na Bill Gates


Leo ni siku ya kimataifa ya watu wanaotumia mkono wa kushoto duniani kote ambayo miaka yote huadhimishwa August 13.
Siku hii maalum ilianzishwa kwa lengo la kutambua mchango na changamoto wanazokumbana nazo watu wanaotumia mkono wa kushoto dhidi ya wale wanaotumia mkono wa kulia.
Zipo facts zilizotolewa Marekani na wanasayansi kuhusu watu wanaotumia mkono wa kushoto nchini humo ambazo zinaweza kusaidia kutumika kama kielelezo kwa watu wengine.

Kwa mujibu wa ripoti ya wanasayansi wa Marekani, 10% ya raia wa nchi hiyo wanatumia mkono wa kushoto.
Utafiti unaonesha kuwa idadi kubwa zaidi ya watu wenye akili yenye uwezo wa ziada ‘Genius’ wanatumia mkono wa kushoto.
Marais watatu kati ya marais watano  wa hivi kariibuni wa Marekani, wanatumia mkono wa kushoto. Yaani Barack Obama, Bill Clinton na Bush Sr.
Watu maarufu waliofanikiwa sana Marekani kama Albert Einstein, Bill Clinton, Oprah Winfrey, Leonardo da Vinci, Barack Obama na Bill Gates wanatumia mkono wa kushoto.
Kama wewe unatumia mkono wa kushoto, hongera.
‘Happy Left-Handers Day

No comments