ads

Breaking News

Rihanna anataka kuinunua Liverpool FC, ashauriwa na Drogba



Mapenzi ya Rihanna kwenye soka yameingia katika hatua nyingine na sasa hataki kuwa shabiki tu bali mmiliki halali wa timu kubwa duniani, na kwa kuanza anataka kuinunua Liverpool FC!
Kwa mujibu wa gazeti la Hispania, El Mundo Deportivo mwimbaji huyo alianza mpango huo muda mfupi baada ya kuisha kwa fainali za kombe la dunia nchini Brazil ambapo alionekana akitweet mara kwa mara kuhusu mechi zilizokuwa zinaendeelea.
Gazeti hilo limeeleza kuwa Rihanna amekuwa akipata ushauri kutoka kwa marafiki zake wa karibu akiwemo mchezaji wa Chelsea, Didier Drogba ili kufanya maamuzi sahihi katika ununuzi wa club ya mpira wa miguu


Kwa sasa Liverpool inamilikiwa na John W. Henry na hana mpango wa kuiuza timu hiyo ya soka.

No comments